ZAIDI YA WAPIGANAJI 18 WAUAWA NA WENGINE 13 KUJERUHIWA WA KUNDI LA TALIBAN, AFGHANNISTAN.


KABUL.

Zaidi ya wapiganaji 18 wa kundi la Taliban wameuawa na wengine 13 kujeruhiwa kwenye mapigano mapya dhidi ya kundi hilo katika mikoa mbalimbali nchini Afghanistan.

Image result for TALIBAN
Kundi la Taliban la Afghanistan.
Gavana wa wilaya ya Imam Sahib mkoani Kunduz, kaskazini mwa nchi hiyo Mahbub Sayyedi amesema wapiganaji wawili wa Taliban waliuawa na wengine watatu kujeruhiwa baada ya vikosi vya usalama vya Afghanistan kukabiliana na washambuliaji hao jana katika kituo cha ukaguzi kilichoko Joy Bigam  wilayani humo.

Habari zinaeleza kuwa wizara ya ulinzi ya Afghanistan leo imesema kuwa wapiganaji 6 wa Taliban waliuawa na wengine 4 kujeruhiwa kwenye mashambulizi ya anga dhidi ya maeneo ya Kajaki na Marja, mkoani Helmand, kusini mwa nchi hiyo.

Wakati huohuo jana katika mkoa wa Farah, magharibi mwa nchi hiyo, wapiganaji 10 wa kundi hilo waliuawa na wengine 6 kujeruhiwa baada ya jeshi la Afghanistan kufanya mashambulizi ya anga na operesheni ya kutokomeza kundi hilo katika wilaya ya Bala Buluk.


ZAIDI YA WAPIGANAJI 18 WAUAWA NA WENGINE 13 KUJERUHIWA WA KUNDI LA TALIBAN, AFGHANNISTAN. ZAIDI YA WAPIGANAJI 18 WAUAWA NA WENGINE 13 KUJERUHIWA WA KUNDI LA TALIBAN, AFGHANNISTAN. Reviewed by safina radio on March 16, 2018 Rating: 5

No comments