ONGEZEKO LA USHINDANI NDANI YA EAC YAKWAMISHA MAUZO YA BIDHAA ZA KENYA.
NAIROBI.
Katibu
mkuu wa Wizara ya viwanda nchini Kenya Bi Betty Maina amesema, Kenya inafanya
juhudi za kuwavutia wawekezaji wa kigeni kuanzisha viwanda nchini humo ili
kuongeza uuzaji wa bidhaa zake katika soko la dunia.
Bi Maina amesema kuwa mauzo
ya bidhaa za Kenya katika nchi za Afrika Mashariki yamekuwa yakikwamishwa
kutokana na kuongezeka kwa ushindani,ingawa Kenya inawatafuta wawekezaji wanaoweza
kutengeneza bidhaa kwa ajili ya soko la kimataifa.
Hata hivyo amesema kuwa Jumuiya
ya Afrika Mashariki EAC ilikuwa ni soko lenye faida kubwa kwa bidhaa za Kenya lakini
sasa nchi hizo zimeanzisha viwanda ambavyo vinatengeneza bidhaa ambazo zilikuwa
zinaagizwa kutoka nchini Kenya.
ONGEZEKO LA USHINDANI NDANI YA EAC YAKWAMISHA MAUZO YA BIDHAA ZA KENYA.
Reviewed by safina radio
on
March 16, 2018
Rating:
No comments