WATU WALIOFARIKI KWA AJALI YA MOTO NCHINI YAFIKIA 64
Serikali ya Urusi leo
imesema kuwa watu waliofariki katika ajali ya moto iliotokea jana katika mji wa
Siberia wa Kemerovo sasa imefikia 64.
Waziri wa masuala ya
dharura Vladmir Puchkov amethibitisha hayo , kufuatia moto ulioliteketeza duka
moja kubwa mjini humo,ambapo watu kadhaa bado hawajulikani waliko.
Moto huo ulitokea
katika jengo la ghorofa nne lenye jina
Winter Cherry umezimwa mapema leo baada ya kuwaka na kuliteketeza jengo hilo
kwa muda wa saa nne.
Chanzo cha moto huo
hakijajulikana,ambapo duka hilo kubwa lililofunguliwa mwaka 2013, lina maeneo
ya sinema kituo cha michezo kwa watoto na bustani ya wanyama.
WATU WALIOFARIKI KWA AJALI YA MOTO NCHINI YAFIKIA 64
Reviewed by safina radio
on
March 26, 2018
Rating:
No comments