MIGUNA MIGUNA AFUKUZWA KWA MARA YA PILI NCHINI KENYA
Hatimaye mwanasisa wa upinzani nchini Kenya, Miguna
Miguna, amefukuzwa kwa mara ya pili tena nchini humo baada ya hapo jana kusafirishwa kwa ndege iliyokuwa ikielekea
Canada.
MIGUNA MIGUNA |
Wakili wa mwanasiasa huyo amethibitisha kufukuzwa tena
kwa Miguna Miguna alipozungumza na shirika lahabari la AFP.
Februari 26, Mahakama ya Juu iliwaamuru maafisa wa
uhamiaji kumruhusu Miguna Miguna arejee nchini Kenya ambapo alirejea Jumatatu
wiki hii.
Akizungumza kwa njia ya simu, Cliff Ombeta, mwanasheria
wa Miguna, amesema mteja wake amepandishwa ndege inayoelekea Dubai lakini
hawakujua ni wapi anapelekwa.
MIGUNA MIGUNA AFUKUZWA KWA MARA YA PILI NCHINI KENYA
Reviewed by safina radio
on
March 29, 2018
Rating:
No comments