JAMII YATAKIWA KUWATUNZA WANYAMA IKIWA NI PAMOJA NA KUWAPATIA HUDUMA ZA AFYA


Jamii imetakiwa kutambua ya kuwa inayo mchango mkubwa wa kuwatunza,kuwathamini na kuwalinda wanyama ikiwa ni pamoja na kuwapatia huduma za afya.


Image result for PICHA YA PUNDA


Hayo yamesemwa na Bw,Livingstone Masija mkurugenzi wa chama cha kutetea na kulinda ustawi wa wanyama mkoani Arusha, Arusha Society For the Protection of Animals (ASPA) wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake kuhusu umuhimu wa wananchi kuwatunza wanyama ili waweze kupata maendeleo kupitia wanyama hao.

 Aidha amesema kuwa kutokana na mpango mkakati wa kidunia wa kupunguza umasikini kwenye jamii kuna baadhi ya wanyama ambao wanatumika katika kufanikisha maendeleo ya millennium akiwemo Punda hii ikiwa na lengo la kurahisisha huduma kwa kijamii.

Ameongeza kuwa watu wote wanatakiwa kuhakikisha kuwa wanyama wanakuwa na afya nzuri kwa kuzingatia chanjo zinazotolewa na serikali kuu pamoja na taasisi mbalimbali zisizo kuwa za kiserikali lengo likiwa ni kuwezesha kuwepo na huduma endelevu ya afya ya wanyama hapa nchini.

Hata hivyo chama cha ASPA, ni chama cha kutetea na kulinda ustawi wa wanyama ambacho kilianzishwa mnamo mwaka 1997 na kushirikiana na serikali pamoja na mashirika mengine katika kutoa elimu juu ya afya ya wanyama.

JAMII YATAKIWA KUWATUNZA WANYAMA IKIWA NI PAMOJA NA KUWAPATIA HUDUMA ZA AFYA JAMII YATAKIWA KUWATUNZA WANYAMA IKIWA NI PAMOJA NA KUWAPATIA HUDUMA ZA AFYA Reviewed by safina radio on March 15, 2018 Rating: 5

No comments