NACTE YATANGAZA UDAHILI KWA WANAFUNZI KATIKA KOZI ZA ASTASHAHADA NA ATASHAHADA.
Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi NACTE limetangaza
udahili kwa wanafunzi katika kozi za Astashahada na Stashahada katika vyuo
vyenye uwezo wa kupokea wanafunzi na kutaka vyuo hivyo kutokusajili wanafunzi
wasiosajiliwa na NACTE.
Akizungumza na waandishi wa Habari jijini Dar es
salaam, Mkuu wa Kitengo cha Udahili katika Baraza hilo, Twaha Twaha, amezitaka
vyuo hivyo mara baada ya kufanya udahili wa wanafunzi kutuma majina NACTE kwa
uhakiki wa sifa na vigezo vya wanafunzi hao katika kozi walizoziomba.
Aidha amesema kuwa Chuo hakitaruhusiwa kumpokea
mwanafunzi yeyote ambaye haja hakikiwa na Baraza la Taifa la Elimu ya
Ufundi-NACTE ili kumuhakikishia mwanafunzi kuwa amedahiliwa kwenye chuo
kinachotambuliwa na kozi anayoisoma kuwa inatambuliwa na Baraza hilo.
Pia, amesema kuwa NACTE imeandaa mfumo mpya
ujulikanao kuwa STUDENTS INFORMATION VERIFICATION SYSTEM yaani Mfumo wa Taarifa
wa Utambuzi wa Wanafunzi.
Hata hivyo, Twaha amewataka wanafunzi wanaoomba
udahili kuhakikisha kuwa wanaomba nafasi katika vyuo ambavyo vimeorodheshwa
katika tovuti ya NACTE ambapo udahili huo umeanza tangu February 20 na
utahitimishwa machi 25 mwaka huu isipokuwa katika kada ya afya kwa vyuo
visivyokuwa vya serikali udahili utahitimishwa Aprili 10.
NACTE YATANGAZA UDAHILI KWA WANAFUNZI KATIKA KOZI ZA ASTASHAHADA NA ATASHAHADA.
Reviewed by safina radio
on
March 23, 2018
Rating:
No comments