UJERUMANI YATAKIWA KUTHIBITISHA KUWA HAITAMRESHA UHISPANIA KIONGOZI WA ZAMANI WA CATALONIA CARLES PUIGDEMONT
Mwanasheria wa kiongozi wa zamani wa jimbo
la Catalonia, Carles Puigdemont, ametoa mwito kwa maafisa nchini Ujerumani
kuthibitisha kwamba hawatamrejesha nchini Uhispania mwanasiasa huyo
anayeshikiliwa hivi sasa nchini Ujerumani.
CARLES PUIGDEMONT |
Mwanasheria huyo, Wolfgang Schomburg,
amelieleza gazeti moja la nchini Ujerumani la the Süddeutsche Zeitung kuwa
Ujerumani inapaswa kuthibitisha hatua hiyo haraka iwezekanavyo kwani vinginevyo
itakuwa inaruhusu migongano ya kimaslahi ya Uhispania nchini Ujerumani.
Schomburg ambaye amewahi kuwa jaji wa
mahakama ya juu nchini Ujerumani amekuwa akimwakilisha Puigdemont tangu
alipotiwa mbaroni kaskazini mwa Ujerumani Jumapili iliyopita wakati alipokuwa
njiani kurejea Ubeligiji akitokea Finland.
UJERUMANI YATAKIWA KUTHIBITISHA KUWA HAITAMRESHA UHISPANIA KIONGOZI WA ZAMANI WA CATALONIA CARLES PUIGDEMONT
Reviewed by safina radio
on
March 29, 2018
Rating:
No comments