WAZIRI MKUU WA UINGEREZA THERESA MAY KUKUTANA NA RAIS WA UFARANSA EMMANUEL MACRON.
Waziri Mkuu wa Uingereza Theresa
May atakutana leo na rais wa Ufaransa Emmanuel Macron baada ya Ufaransa kusema
ni mapema mno kuamua iwapo hatua inatakiwa kuchukuliwa kufuatia shambulizi
dhidi ya jasusi wa zamani wa Urusi Sergei Skripal na mtoto wake wa kike nchini
Uingereza.
WAZIRI MKUU WA UINGEREZA THERESA MAY |
Ufaransa imesema leo inakubaliana
na Uingereza kwamba Urusi ilihusika katika shambulizi la sumu dhidi ya jasusi
wake wa zamani huko England.
Wakati haya yakiarifiwa Urusi
imesema bado iko tayari kushirikiana na Uingereza kuchunguza shambulizi hilo
dhidi ya afisa wake wa zamani wa ujasusi.
RAIS WA UFARANSA EMMANUL MACRON |
Hata hivyo Uingereza imesema
itawafukuza maafisa 23 wa kidiplomasia wa Urusi na kuiwekea vikwazo nchi hiyo
kwa kumwekea gesi ya sumu Skripal na mtoto wake wa kike, madai ambayo Urusi
inayakanusha.
WAZIRI MKUU WA UINGEREZA THERESA MAY KUKUTANA NA RAIS WA UFARANSA EMMANUEL MACRON.
Reviewed by safina radio
on
March 15, 2018
Rating:
No comments