DK. TIZEBA ATOA AGIZO KWA MTENDAJI MKUU WA NFRA KUNUNUA MAZAO YA WAKULIMA KWA WAKATI.
ARUSHA.
Waziri wa Kilimo hapa nchini Dk. Charles Tizeba
amemwagiza Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ghala la Chakula Nchini NFRA kuhakikisha
kuwa wananunua mahindi kwa wakulima kila wanapouza mazao wanayoyahifadhi katika
maghala hayo hapa nchini.
Waziri wa kilimo Dk. Charles Tizeba. |
Dk. Tizeba ametoa agizo hilo jijini Arusha wakati
alipokuwa akitembelea ghala la chakula la kanda ya Arusha ambapo amesema
utaratibu wa wakala kununua mahindi kwa msimu umesababisha hasara kwa kuwa
hujipangia bei ya kununua.
Aidha, amesema kuwa NFRA wasisubiri mpaka msimu wa
mwezi Julai kwa ajili ya kununua mazao ya wakulima kwani hali hiyo inachangia
mazao ya wananchi kurundikana na kusababisha bei kushuka.
Pia, ameitaka Wakala hao kuondokana na utaratibu huo
wa kusubiri muda Fulani ili kununu mahindi bali wanunue mahindi wakati wowote
pamoja na kuhakiki mazao hayo ili kubaini kasoro zilizopo.
Hata hivyo Waziri Tizeba ametumia nafasi hiyo
kuwatahadharisha wakuu wote wanaosimamia Maghala ya Chakula ya Taifa kuwa
yeyote atakaye zembea kuuza mazao ya chakula aliyonayo hatua kali zitachukuliwa
dhidi yake.
DK. TIZEBA ATOA AGIZO KWA MTENDAJI MKUU WA NFRA KUNUNUA MAZAO YA WAKULIMA KWA WAKATI.
Reviewed by safina radio
on
March 15, 2018
Rating:
No comments