SHAMBULIZI LASABABISHA VIFO VYA WATU 37 MASHARIKI MWA GHOUTA.


Mashambulizi yanayoendelea kufanywa na jeshi la Assad mashariki mwa ghouta yamesababisha vifo vya watu 37 na wengine kujeruhiwa.


Kwa mujibu wa habari,raia 37 wakiwemo wanawake na watoto wamepoteza maisha kwa kuunguzwa na mabomu yaliyorushwa na Assad katika amshambulizi hayo.
Jeshi la Assad limekuwa likishirikiana na Urusi kufanya mashambulizi hayo nchini Syria.
Ripoti zinaonesha kuwa idadi ya vifo inaweza kuwa kubwa zaidi kwani mashambulizi bado hayajasitishwa.
Licha ya Umoja wa Mataifa kuitaka Syria kuachana na mashambulizi hayo,jeshi la Assad linaonekana kutokuwa na nia ya kufuata maagizo hayo.







SHAMBULIZI LASABABISHA VIFO VYA WATU 37 MASHARIKI MWA GHOUTA. SHAMBULIZI LASABABISHA VIFO VYA WATU 37 MASHARIKI MWA GHOUTA. Reviewed by safina radio on March 23, 2018 Rating: 5

No comments