MAGAIDI 7 WA AL-SHABABU WAUAWA, KISMAYU.


MOGADISHU.

Jeshi la Somalia limewaua wapiganaji 7 wa kundi la Al-Shabaab mjini Kismayu, Kusini mwa nchi hiyo.

Image result for Jeshi la Somalia
Jeshi la Somalia.
Kamanda wa jeshi la serikali mjini Kismayu, Bw. Mukhtar Abdi amesema, operesheni hiyo ya kijeshi imefanywa baada ya jeshi hilo kupata habari kuwa kundi la Al-Shabaab linapanga kufanya mashambulizi katika eneo la Wirkoy.

Bw. Abdi pia amesema, askari mmoja wa jeshi hilo amejeruhiwa katika operesheni hiyo, na mapambano dhidi ya kundi la Al-Shabaab kusini mwa nchi hiyo yataendelea.



MAGAIDI 7 WA AL-SHABABU WAUAWA, KISMAYU. MAGAIDI 7 WA AL-SHABABU WAUAWA, KISMAYU. Reviewed by safina radio on March 15, 2018 Rating: 5

No comments