RAIS MAGUFULI AZINDUA JIWE LA MSINGI LA UJENZI WA RELI YA KATI YA MWENDO KASI YA STANDARD GAURGE.
DODOMA.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John
Magufuli amezindua jiwe la msingi la ujenzi wa reli ya kati ya mwendo kasi ya
Standard Gaurge inayotoka Matoporwa-Morogoro hadi Ihumwa mkoani Dodoma.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Magufuli. |
Akizungumza katika uzinduzi huo uliohudhuriwa na
viongozi mbali mbali wa kiseikali kutoka ndani na nje ya nchi, Rais Magufuli
amesema kuwa mradi huo wa awamu ya pili unagharamiwa kwa fedha za watanzania
kwa zaidi ya shilingi trilioni 7.
Aidha, amesema kuwa mradi huo unatarajiwa kuwaajiri
watanzania zaidi ya elfu thelathini kuwa wafanyakazi wa kudumu na wafanyakazi
elfu sita wasio wa kudumu katika kutekeleza mradi huo.
Pia, amesema kuwa serikali ya awamu ya tano imejibu
suala la ajira kwa vitendo ambapo ameelezea miradi mbali mbali mikubwa iliyoanzishwa
na serikali katika kuleta maendeleo ya nchi ikiwemo mradi wa umeme wa Stilllers
George, usambazaji wa umeme vijijini- REA, na kutengenezwa kwa Meli kubwa
katika ziwa Victoria.
Hata hivyo, amewataka wananchi kuwa wazalendo katika
kulipa kodi ili kuharakisha maendeleo ya nchi huku akiitaka Mamlaka ya
Ukusanyaji Kodi Tanzania-TRA kuhakikisha kuwa inatoa elimu kwa wananchi kwa
ajili ya kuondoa tabia ya ukwepaji wa malipo ya kodi.
RAIS MAGUFULI AZINDUA JIWE LA MSINGI LA UJENZI WA RELI YA KATI YA MWENDO KASI YA STANDARD GAURGE.
Reviewed by safina radio
on
March 14, 2018
Rating:
No comments