TRUMP AMPONGEZA PUTIN
Rais wa Marekani Donald Trump amempongeza Rais wa Urusi
Vladmir Putin kwa kushinda muhula wa nne madarakani katika uchaguzi uliofanyika
Jumapili iliyopita.
RAIS TRUMP |
Trump amesema amempigia simu Putin kumpongeza kwa ushindi huo
na pia kujadili uwezekano wa kuandaa mkutano wa kilele kati yao katika siku za
hivi karibuni.
Viongozi hao wawili pia wamejadili umuhimu wa kuwa na juhudi
za pamoja za kupunguza ushindani wa kuoneshana nguvu za kijeshi, kuimarisha
uchumi, mizozo ya Ukraine na Syria na pia wamejadili mpango wa kinyuklia wa
Korea Kaskazini.
Hata hivyo hawakujadili suala la Urusi kudaiwa kuhusika
katika kumshambulia Sergei Skripal, jasusi wa zamani wa Urusi anayeishi
Uingereza ambapo Nchi za magharibi zimeghadhabishwa na shambulizi hilo la
kutumia silaha za sumu.
Naye Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong Un pia amempongeza
Rais Putin na kumtakia kila la kheri katika kulijenga taifa lenye nguvu zaidi.
TRUMP AMPONGEZA PUTIN
Reviewed by safina radio
on
March 21, 2018
Rating:
No comments