UN YAONGEZEA MUDA UNMISS, SUDAN KUSINI.
JUBA.
Baraza
la usalama la Umoja wa Mataifa limepitisha uamuzi wa kuiongezea muda tume
maalumu ya Umoja huo nchini Sudan Kusini UN MISS hadi tarehe 15, Machi mwakani
katika zoezi la kutokomesha vita nchini humo.
Walinda amani katika ujumbe wa umoja wa mataifa nchini Sudan Kusini, UNMISS. |
Uamuzi huo umezitaka pande
mbalimbali za Sudan Kusini zisimamishe vita mara moja, na kusema kuwa baraza la
usalama litafikiri kuchukua hatua zote na kuwaadhibu watu wanaovuruga amani,
utulivu na usalama wa Sudan Kusini.
Habari zinaeleza kuwa uamuzi
huo pia umeamua kudumisha ukubwa wa tume hiyo iliyo na askari wasiozidi elfu kumi
na saba na polisi elfu mbili mia moja na moja.
Askari
hao watakuwa pamoja na wale wa kikosi cha ulinzi cha kikanda kitakachoundwa
chini ya idhini ya katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa, lakini hakitakuwa na askari
zaidi ya elfu 4.
UN YAONGEZEA MUDA UNMISS, SUDAN KUSINI.
Reviewed by safina radio
on
March 16, 2018
Rating:
No comments