IMEBAINISHWA KUNA UMUHIMU WA KUFANYA UKOMBOZI WA KISIGINO


Imebainishwa kuwa kuna umuhimu mkubwa wa kila mtu kufanya ukombozi wa kisigino chake kwakuwa adui amekuwa akitumia kisigino cha mguu wa mtu kuharibu kusudi la Mungu na kumfanya kupoteza muelekeo wa maisha.



Image result for picha ya kisigino cha mtu


Huduma ya redio safina kesho katika ukumbi wa maombi uliopo mbauda jijini Arusha kuanzia saa mbili asubuhi hadi saa sita mchana imekuandalia maombi maalumu ya mwendelezo wa kuchovya miguu kwenye mafuta pamoja na kuwaombea watoto ili Mungu aweze kuwaweka mbali na vifungo malimbali katika maisha yao.

Aidha kwa mujibu wa somo hilo wapo watu ambao wameendelea kutaabika na magonjwa,kutokupata kazi hatakama wamesoma,migogoro katika ndoa,kukosa watoto,mimba kuharibika au kupata watoto wa jinsia moja kutokana na adui kukamata visigino vya miguu na kuharibu misingi ya maisha yao.

Vile live katika maombi hayo ya mwendelezo wa kuchovya miguu kwenye mafuta pia kutafanyika maombi kwaajili ya watoto ambao ni wakorofi wasio wasikiliza wazazi wavuta bangi,wezi,watoto wasiopenda kwenda shule pamoja na watoto wachanga ambao wanalia nyakati za usiku.

Hata hivyo kesho katika ukumbi wa maombi wa safina redio uliopo mbauda jijini Arusha kila atapaswa kuja na kitambaa kwaajili ya kufanya kitendo cha imani.

IMEBAINISHWA KUNA UMUHIMU WA KUFANYA UKOMBOZI WA KISIGINO IMEBAINISHWA KUNA UMUHIMU WA KUFANYA UKOMBOZI WA KISIGINO Reviewed by safina radio on March 19, 2018 Rating: 5

No comments