DK. TIZEBA AMUAGIZA MRAJISI MSAIDIZI WA NCU KILIMANJARO KUWASILISHA MIKATABA YA WAWEKEZAJI KATIKA SHAMBA LA LA KIBO AND KIKAFU ESTATE.


KILIMANJARO.

Waziri wa Kilimo Hapa nchini Dk. Charles Tizeba amemwagiza Mrajisi Msaidizi wa ushirika Mkoani Kilimanjaro kuwasilisha mikataba ya wawekezaji katika Shamba la Kibo and Kikafu Estate lililopo wilayani Hai mkoani humo. 

Image result for aziri wa Kilimo Dk. Charles Tizeba
Waziri wa KilimoDk. Charles Tizeba.

Akizungumza mkoani humo wakati alipomtembelea mwekezaji huyo Dk. Tizeba amesema kuwa hawezi kumvumilia mwekezaji asiyekuwa na Mkataba wa Uwekezaji.

Waziri huyo ametaka suala hilo lifanyike mara moja licha ya muda waliyojiwekea  huku akisema kuwa mtu hawezi kuwekeza fedha mahali ambapo hana mkataba nakumtaka mwekezaji huyo kupeleka mkataba wake na sambamba na mkataba wa mwekezaji wa kwanza.

Naye Mwekezaji wa Shamba hilo Shrevod Givodi amesema kuwa ameshindwa kuwa na mkataba kutokana na kushindwa kupata muafaka katika majadiliano na ofisi ya mkoaa na mwekezaji aliyeondoka.

Vile vile, Dk. Tizeba ametembelea mashamba ya kahawa ya Kilimanjaro Plantation na Chama Kikuu cha Ushirika mkoani Kilimanjaro NCU.



DK. TIZEBA AMUAGIZA MRAJISI MSAIDIZI WA NCU KILIMANJARO KUWASILISHA MIKATABA YA WAWEKEZAJI KATIKA SHAMBA LA LA KIBO AND KIKAFU ESTATE. DK. TIZEBA AMUAGIZA MRAJISI MSAIDIZI WA NCU KILIMANJARO KUWASILISHA MIKATABA YA WAWEKEZAJI KATIKA SHAMBA LA LA KIBO AND KIKAFU ESTATE. Reviewed by safina radio on March 14, 2018 Rating: 5

No comments