VALDS DOMBROVSK AAHIDI KUIPA USHIRIKIANO UINGERERA DHIDI YA SHAMBULIZI LA SUMU KWA JASUSI WA ZAMANI WA URUSI.


BRUSSELS.
Umoja wa Ulaya umeahidi kuipa ushirikiano Uingereza kufuatia nchi hiyo kuituhumu Urusi kuhusika na shambulizi la sumu dhidi ya jasusi wa zamani wa Urusi pamoja na binti yake.
Ahadi hiyo inakuja baada ya kutolewa na makamu wa rais wa halmashauri ya Ulaya Valdis Dombrovskis wakati kukiwa na wasiwasi nchini Uingereza kuhusu ushirikiano wa kiusalama baada ya nchi hiyo kujiondoa kwenye Umoja wa Ulaya mwishoni mwa Machi 2017.
Image result for makamu wa rais wa halmashauri ya Ulaya Valdis Dombrovskis
Makamu wa rais wa halmashauri ya Ulaya Valdis Dombrovskis.
Naye msemaji wa mkuu wa sera za nje wa Umoja wa Ulaya Federeca Moghereni amelielezea shirika la habari la Reuters kuwa matumizi ya silaha za sumu katika jaribio la kuwaua raia nchini Uingereza ni suala linaloshtua.
Hata hivyo, ameongeza kuwa Umoja wa Ulaya unaungana na Uingereza katika kuhakikisha kuwa haki inapatikana pamoja na kuahidi kutoa ushirikiano itakapolazimu kutoa ushirikiano dhidi ya uchunguzi huo.


VALDS DOMBROVSK AAHIDI KUIPA USHIRIKIANO UINGERERA DHIDI YA SHAMBULIZI LA SUMU KWA JASUSI WA ZAMANI WA URUSI. VALDS DOMBROVSK AAHIDI KUIPA USHIRIKIANO UINGERERA DHIDI YA SHAMBULIZI LA SUMU KWA JASUSI WA ZAMANI WA URUSI. Reviewed by safina radio on March 14, 2018 Rating: 5

No comments