HUDUMA YA REDIO SAFINA YAANDAA MAALUMU YA UKOMBOZI YA KUFUNGUA MILANGO YA MIGUU.
ARUSHA.
Imeelezwa kuwa milango ya miguu ya mtu inaweza
kufungwa kupitia viapo mbalimbali vinavyowekwa na wakuu wa makabila pamoja na
ukoo nakumfanya mtu kushindwa kufanya jambo lolote la msingi kutokana na
kuwekewa mipaka kiroho na kiuchumi.
Huduma ya redio safina kesho katika ukumbi wa maombi
uliopo mbauda jijini Arusha kuanzia saa mbili hadi saa sita mchana imekuandalia
maombi maalumu ya ukombozi wa kufungua milango ya miguu katika ulimwengu wa
kiroho ili watu wawekwe huru mbali na viapo vinavyowatesa.
Ukombozi wa kufungua milango ya miguu katika ulimwengu wa kiroho ili watu wawekwe huru mbali na viapo vinavyowatesa.
Aidha milango ya miguu ya mtu inapofungwa na viapo
vya ukoo au kabila lake hushindwa kutambua majira na nyakati sahihi za kusoma kufanya
biashara,kilimo,kufuga au kufanya uvuvi kutokana na ufahamu wake kutekwa na
kutumikishwa kinyume na kusudi la Mungu.
|
Kwa mujibu wa somo hilo la kufungua milango iliyofungwa
kwa viapo vya wakuu wa makabila pamoja na ukoo watu wengi wamewekewa mipaka
katika eneo la kuoa au kuolewa kupangiwa idadi ya watoto katika ndoa kupatwa na
magonjwa ya kurithi, kufilisika na mara nyingine mtu kupoteza maisha.
Hata hivyo siku ya kesho katika ukumbi wa maombi
uliopo mbauda jijini Arusha kutafanyika
kitendo cha imani cha kuchovya miguu kwenye mafuta ili kutakaswa na kufunguliwa
milango ya miguu katika ulimwengu wa kiroho ili kufanikiwa.
HUDUMA YA REDIO SAFINA YAANDAA MAALUMU YA UKOMBOZI YA KUFUNGUA MILANGO YA MIGUU.
Reviewed by safina radio
on
March 16, 2018
Rating:
No comments