RAIS MAGUFULI AWAAPISHA MABALOZI WAWILI
Rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania Mh John
Magufuli leo amewaapisha mabalozi wawili ambao watawakilisha Tanzania katika
nchi za Rwanda na Urusi.
RAIS MAGUFULI KUSHOTO AKIMWAPISHA ERNEST MANGU |
Mabalozi hao walioapishwa Ikulu jijini Dar-es-salaam
ni Inspekta Jenerali mstaafu wa jeshi la polisi Ernest Mangu ambaye anakwenda
kuwa balozi wa Tanzania nchini Rwanda na Meja Jenerali mstaafu Saimon Marko ambaye
anakuwa balozi wa Tanzania nchini Urusi.
Akizungumza mara baada ya kuapishwa kwa mabalozi hao
makamu wa rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania Mh Samia Suluhu Hassan
amewataka mabalozi hao kwenda kuwakilisha nchi vizuri katika mataifa wanayokwenda
kwa manufaa ya nchi zote.
Kwa upande wake naibu waziri wa mambo ya nje,Afrika
Mashariki kikanda na kimataifa Mh Suzan Kolimba amesema kuwa wizara yake iko
tayari kuwapa ushirikiano mabalozi hao ili wakafanye kazi zao vizuri katika
nchi walizoteuliwa kwa kujali uzalendo,uaminifu na weledi.
Naye balozi wa Tanzania nchini Rwanda IGP mstaafu
Ernest Mangu amesema kuwa atatumia nguvu na akili zake zote katika kutekeleza
majukumu yake ya kibalozi ambaye ameainishwa kwenye sheria na taratibu
mbalimbali za nchi.
Hata hivyo hafla ya kuapishwa kwa mabalozi hao
zilihudhuriwa na viongozi mbalimbali akiwemo katibu mkuu kiongozi Balozi John
Kijazi,watendaji wa serikali na wakuu wa ulinzi na usalama.
RAIS MAGUFULI AWAAPISHA MABALOZI WAWILI
Reviewed by safina radio
on
March 21, 2018
Rating:
No comments