JAMII IMETAKIWA KUFAHAMU KUWA KUNA UWEZEKANO MKUBWA WA KUVUNJA VIAPO VYA ROHO YA MAUTI KWA NJIA YA MAOMBI YA KUFUNGA PAMOJA NA KUTUMIA DAMU YA YESU KWA IMANI.
Jamii imetakiwa kufahamu kuwa kuna
uwezakano mkubwa wa kuvunja viapo vya roho ya mauti kwa njia ya maombi ya
kufunga pamoja na kutumia damu ya yesu kwa imani.
Huduma ya redio safina Siku ya kesho
katika ukumbi wa maombi uliopo mbauda hapa jijini Arusha kuanzia saa mbili
asubuhi hadi saa sita mchana imekuandalia maombi ya kuhitimisha somo la kuvunja
viapo vya mauti ndani ya jamii.
Aidha pamoja na viapo hivyo vya mauti
kuleta madhara makubwa ndani ya jamii imebainika kuwa damu ya Yesu ina uwezo wa
kuondoa viapo hivyo ikiwa watu wataitumia damu hiyo ipasavyo kwa imani na
kuomba kwa bidii.
Hata hivyo katika maombi haya ya
kuhitimisha somo la kuvunja viapo vya mauti watu watafundishwa namna ya kutumia
damu ya Yesu kwa imani kuvunja viapo hivyo ambapo pia watu wataombewa ili
waweze kufunguliwa kwenye vifungo mbalimbali vinavyowatesa yakiwemo magonjwa
sugu,laana,migogoro ya ndoa,pamoja na tatizo la ukosefu wa ajira.
JAMII IMETAKIWA KUFAHAMU KUWA KUNA UWEZEKANO MKUBWA WA KUVUNJA VIAPO VYA ROHO YA MAUTI KWA NJIA YA MAOMBI YA KUFUNGA PAMOJA NA KUTUMIA DAMU YA YESU KWA IMANI.
Reviewed by safina radio
on
February 16, 2018
Rating:

No comments