KATIBU MKUU WA SERIKALI YA MAPINDUZI ZANZIBAR DK.ABDUL HAMID MZEE AMESEMA VIONGOZI WA SERIKALI WANATAKIWA KUWA NA UWEZO WA KUJADILI MIKATABA


TAREHE 20-02-2018


Katibu Mkuu Kiongozi wa serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Dk. Abdul Hamid Mzee amesema viongozi wa serikali wanapaswa kuwa na uwezo wa kujadili mikataba kabla ya kusaini ili kuondoa changamoto zinazoweza kujitokeza.

Akizungumza Mjini Unguja wakati wa mafunzo ya siku mbili ya kuwajengea uwezo Makatibu Wakuu na Manaibu wao kutoka wizara mbali mbali za serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Dk. Mzee amesema kuwa kosa dogo linapotokea wakati wa kutia saini mikataba linaweza kulisababishia taifa hasara.

Aidha, Dk. Mzee amesema kuwa kunakosekana utaalamu unaohitajika wa kushughulika katika kusaini mikataba kutokana na kufanya kazi kwa  mazoea huku ulimwengu ukiwa unabadilika na wenye wajanja wengi hivyo watendaji lazima wajengewe uwezo wa namna ya kukabiliana na suala hilo hasa wanaposaini mikataba na makampuni makubwa yenye uzoefu wa mda mrefu katika kazi.

Halikadhalika amebainisha kuhusiana na uwepo wa uvumbuzi wa mafuta na gesi visiwani Zanzibar kutokana na Swala hilo kuwa jipya na halijawahi kufanyika wisiwani humo ambapo watendaji wanaweza kukutana na makampuni makubwa yaliyodumu kwa zaidi ya miaka 50 katika kazi hiyo.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Mafunzo ya Uongozi inayoongoza mafunzo hayo ya kuwajengea uwezo watedaji hao wa Zanzibar, Kadari Singo amesema kuwa wanawajenga viongozi katika maeneo makuu watatu ambapo kiongozi anapaswa kuwa na maamuzi ya kimkakati, kusimamia rasilimali za nchi inavyopaswa, na kujijengea sifa binafsi za uongozi.

KATIBU MKUU WA SERIKALI YA MAPINDUZI ZANZIBAR DK.ABDUL HAMID MZEE AMESEMA VIONGOZI WA SERIKALI WANATAKIWA KUWA NA UWEZO WA KUJADILI MIKATABA KATIBU MKUU WA SERIKALI YA MAPINDUZI ZANZIBAR DK.ABDUL HAMID MZEE AMESEMA VIONGOZI WA SERIKALI WANATAKIWA KUWA NA UWEZO WA KUJADILI MIKATABA Reviewed by safina radio on February 20, 2018 Rating: 5

No comments