SERIKALI YA MAGU YAIOMBA SERIKALI IWATATULIE KERO YA MAJI.
MWANZA.
Taarifa ya Habari saa 01:00 mchana, 14 February, 2018.
![]() |
Bw. George Lutengano Mwalwiba, Mkurugenzi wa Halimashauri ya Wilaya Magu. |
Imeelezwa kuwa Wilaya ya Magu mkoani
Mwanza yenye wakazi zaidi ya laki tatu inakabiliwa na changamoto ya upatikanaji
wa maji hali ambayo imewafanya wananchi wake kuomba serikali iwatatulie kero
hiyo.
Mkurugenzi wa Halimashauri ya Magu George Lutengano Mwalwiba amekiri kuwepo kwa changamoto hiyo na kuongeza kuwa kwa sasa
wanaendelea kutekeleza miridi mbalimbali ili kukabiliana na changamoto hiyo ya
upatikanaji wa maji.
Naye, Kaimu Mhandisi wa maji Wilaya ya
Magu Richard Mlilwa amesema kuwa changamoto hiyo imewalazimu kubuni miradi ya
visima vya maji vinavyotumia nishati ya jua vinavyosaidia kutatua tatizo hilo
la maji, kauli iliyoungwa mkono na mwenyekiti wa kamati ya maji toka moja ya
vijiji vinne vyenye miradi hiyo.
Takwimu za upatikanaji wa maji katika
wilaya ya Magu mkoani Mwanza zinaonesha kwamba katika maeneo ya vijijini maji
yanapatikana kwa asilimia 45 na eneo la mjini inapatikana kwa asilimia 20
pekee.
SERIKALI YA MAGU YAIOMBA SERIKALI IWATATULIE KERO YA MAJI.
Reviewed by safina radio
on
February 14, 2018
Rating:

No comments