WAPIGANAJI WA KIKURDI NCHINI SYRIA WAMEWAKAMATA WANAMGAMBO WAWILI WA UINGEREZA WA KUNDI LA IS
TAREHE 09-02-2018
Wapiganaji wa kikurdi nchini Syria wamewakamata
wanamgambo wawili wa Uingereza wa kundi linalojiita Dola la Kiislamu - IS
wanaojulikana kwa jukumu lao katika mateso na mauaji ya mateka wa nchi za
magharibi.
Maafisa wa Marekani wamesema wapiganaji hao
wawili wametambuliwa kuwa Alexanda Kotey na El Shafee Elsheikh ambao walikuwa wanachama wawili wa mwisho wa
kikundi kinachojiita Beatles cha wanamgambo wanne wa Uingereza waliokuwa
mafichoni.
Habari zinaeleza kuwa Kiongozi wa wawili hao
amejulikana kama Mohammed Emwazi, ambaye ni raia wa Uingereza mwenye asili ya
Kiarabu.
Jihadi John, kama alivyofahamika, alionekana
akiwaua mateka, wakiwemo wanahabari wa Marekani Steven Sotloff na James Foley, ambapo
video kadhaa za IS zilizoonesha watu wakikatwa vichwa.
Habari
za kukamatwa Kotey na Elsheikh ziliripotiwa kwanza na gazeti la New York Times,
ambalo lilisema watu hao wawili wanazuiliwa na wanajeshi wa Kikurdi nchini
Syria wanaoungwa mkono na Marekani katika ngome za mwisho za wanamgambo wa IS
nchini Syria kwenye Mto wa Euphrates kusini mwa mpaka na Iraq.
WAPIGANAJI WA KIKURDI NCHINI SYRIA WAMEWAKAMATA WANAMGAMBO WAWILI WA UINGEREZA WA KUNDI LA IS
Reviewed by safina radio
on
February 09, 2018
Rating:
No comments