AL SHABAB YAWASHAMBULIA AMISOM
Kundi la Al Shabab nchini Somalia limetekeleza
mfululizo wa mashambulizi dhidi ya askari wa kikosi cha Umoja wa Afrika
(Amisom) na jeshi la Somalia katika mkoa wa Shabelle, kusini mwa Mogadishu.

Kundi hilo linasema kuwa lilitekeleza
mashambulizi kadhaa dhidi ya kambi za kikosi hicho kinachosimamia amani na
usalama nchini Somalia.
Kundi la Al Shabab linasema liliwaua askari 59
wa Amisom, wengi wao ni kutoka Uganda, na lilipoteza wapiganaji wake 14 katika
vita hivyo huku jeshi la Uganda likisema kuwa wamepoteza askari wake wanne na wamefaulu kuua magaidi
22.
Afisa wa jeshi la Somalia, Farah Osman, ambaye
alinukuliwa na shirika la habari la Reuters leo asubuhi amesema magari mawili
yaliyokua yametegwa mabomu yalianza kulipukia magari ya tume ya Umoja wa Afrika
na yale ya jeshi la Somalia.
Hata hivyo, shambulio hilo la jana dhidi ya
kambi ya Bulomarer, kilomita 130 kusini magharibi mwa Mogadishu, liligharimu
maisha ya askari kadhaa wa Amisom, kwa mujibu wa mashahidi.
AL SHABAB YAWASHAMBULIA AMISOM
Reviewed by safina radio
on
April 02, 2018
Rating:
No comments