WHITE HOUSE YASEMA UTAWALA WA TRUMP UMEFANYA MAZUNGUMZO NA KOREA KASKAZINI.


Ikulu ya Marekani White house imesema kuwa utawala wa Rais Donald Trump umefanya mazungumzo ya ngazi ya juu na Korea Kaskazini, ingawa hakujakuwepo mawasiliano ya moja kwa moja kati ya Rais Trump na kiongozi wa Korea Kaskazini, Kim Jong Un.

Image result for White house

Gazeti la Washington Post limeripoti kuwa mkuu wa shirika la ujasusi la Marekani CIA Mike Pompeo alifanya safari ya siri mjini Pyongyang wiki ya kwanza ya mwezi Aprili mwaka huu na kukutana na Kim.

Vyanzo vyenye taarifa kuhusu ziara hiyo, vimenukuliwa na gazeti hilo, vikieleza kuwa mazungumzo hayo yamelenga juu ya maandalizi ya mkutano wa kilele baina ya Trump na Kim unaotarajiwa kufanyika siku chache zijazo.

Mazungumzo ya ngazi ya juu kati ya nchi hizo mbili pia yamethibitishwa na Rais Trump katika mkutano na Waziri Mkuu wa Japan, Shinzo Abe katika jimbo la Florida.

Trump amesema anaridhia majadiliano ya kumaliza rasmi vita vya Korea.

WHITE HOUSE YASEMA UTAWALA WA TRUMP UMEFANYA MAZUNGUMZO NA KOREA KASKAZINI. WHITE HOUSE YASEMA UTAWALA WA TRUMP UMEFANYA MAZUNGUMZO NA KOREA KASKAZINI. Reviewed by safina radio on April 18, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.