UJERUMANI NA IRAQ KUSHIRIKIANA KUWARUDISHA NYUMBANI WAKIMBIZI


Waziri wa maendeleo wa Ujerumani Gerd Müller amesema nchi yake na Iraq zitashirikiana katika kutekeleza zoezi la kuwarudisha nyumbani wakimbizi wa Iraq.

Image result for PICHA YA GERD MULLER WAZIRI WA ULINZI WA UJERUMANI
GERD MULLER
Waziri Müller amesema wakimbizi elfu kumi wa Iraq walioko nchini Ujerumani watasaidiwa ili waweze kurudi kwao,ambapo amesema  Ujerumani na Iraq zimekuabliana kushirikiana kwa undani zaidi ili kuwasaidia kurudi nyumbani Wairaki wanaoomba hifadhi ya ukimbizi nchini Ujerumani.

Waziri huyo wa maendeleo wa Ujerumani aliyefanya ziara nchini Iraq pia amesema Ujerumani na Iraq zitafanya kazi kwa pamoja ili kuwapa fursa za elimu na ajira Wairaki wanaorejea nchini kwao.

Hata hivyo Kati ya wairaki elfu ishirini na nne wanaoishi nchini Ujerumani kwa sasa,12,000 hawajafanikiwa kupata hifadhi ya ukimbizi.


UJERUMANI NA IRAQ KUSHIRIKIANA KUWARUDISHA NYUMBANI WAKIMBIZI UJERUMANI NA IRAQ KUSHIRIKIANA KUWARUDISHA NYUMBANI WAKIMBIZI Reviewed by safina radio on April 23, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.