WATU 10 WAMEFARIKI NCHINI CANADA

Watu kumi wamepoteza maisha baada ya mwanaume mmoja aliyekuwa akiendesha gari kugonga umati wa watu katika jiji la Toronto nchini Canada,tukio ambalo polisi imeliita shambulizi la makusudi.
Gari lililoua watu huko Canada
GARI LILILOUA WATU 
Kisa hicho kimetokea jana katika eneo lenye umbali wa kilomita 16 kutoka ukumbi wa mkutano wa mawaziri wa mataifa makubwa kiviwanda G7.
Mkuu wa polisi katika jiji hilo Mark Saunders amethibitisha idadi ya vifo na kusema shambulizi hilo lilikuwa la makusudi lakini tukio hilo halihusiani na mkutano huo.
Waziri wa usalama wa Canada Ralph Goodale amewaambia waandishi wa habari kwamba ni mapema kusema tukio hilo ni la kigaidi.
Kumekuwa na matukio ya magari makubwa kutumiwa na magaidi na kusababisha vifo katika maeneo yenye mikusanyiko
WATU 10 WAMEFARIKI NCHINI CANADA WATU 10 WAMEFARIKI NCHINI CANADA Reviewed by safina radio on April 24, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.