WANANCHI WOTE WANAOISHI MABONDENI NCHINI WATAKIWA KUONDOKA.


Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh Majaliwa Kasim Majaliwa amewataka wananchi wote waishio mabondeni kote nchini kuondoka mara moja ili kuepukana na majanga yanayotokana na mvua zinazoendelea kunyesha.

Image result for PICHA YA WAZIRI MKUU MAJALIWA
WAZIRI MKUU MAJALIWA.

Waziri Mkuu Majaliwa ametoa maagizo hayo leo bungeni mjini Dodoma wakati akijibu maswali ya papo kwa papo kwa waziri mkuu ambapo amesema kuwa maafa yaliyo sababishwa na mafuriko ya maji ya mvua  ni makubwa kwani hadi sasa wako waliopoteza maisha na wengine nyumba zao kusombwa na maji.

Aidha Mh Majaliwa amesema kuwa yapo maeneo ya bondeni ambayo yameathiriwa na mvua huku shughuli za uokozi zikiwa ni changamoto kutokana na maeneo hayo kutokupitika kwa urahisi kutokana na miundombinu mibovu iliyopo.

Amesema kuwa pamoja na madhara makubwa yanayotokana na mvua tayari serikali kupitia wizara ya ofisi ya makamu wa rais muungano na mazingira pamoja na ofisi ya rais TAMISEMI imeandaa miradi ya kuboresha miundombinu ya barabara na mifereji ya kusafirisha maji katika mikoani ikiwemo jiji la Dar-es-salaam.

Hata hivyo amewataka wabunge kutoingiza suala la siasa katika zoezi hilo la wananchi kuondoka mabondeni bali wawahamasishe kuhama kwa kuwa serikali inaandaa fedha ya kuboresha miundombinu katika  maeneo yote ya mabondeni ili maji yaweze kupi
ta kwa urahisi na kuepukana na majanga ya mvua.

WANANCHI WOTE WANAOISHI MABONDENI NCHINI WATAKIWA KUONDOKA. WANANCHI WOTE WANAOISHI MABONDENI NCHINI WATAKIWA KUONDOKA. Reviewed by safina radio on April 19, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.