MITI ELFU MBILI MIA TANO IMEPANDWA KATIKA MSITU WA CHOME SHENGENA


Ili kuzua uharibifu wa mazangira katika msitu wa Chome Shengena ulioko katika wilaya ya Same mkoani Kilimanjaro serikali imepanda miti elfu mbili mia tano katika msitu huo kati ya mwaka wa 2012 hadi 2017.

Image result for PICHA YA MSITU WA CHOME SHENGENA WILAYANI SAME MKOANI KILIMANJARO


Hayo yameelezwa leo bungeni mjini Dodoma na naibu waziri wa nchini ofisi ya makamu wa rais muungano na mazingira Mh Kangi Lugola wakati akijibu swali la mbunge wa Same Mashariki Mh Nangejwa Kaboyoka aliyetaka kujua serikali ina mpango gani wa kuzuia uharibifu wa mazingira unaoendelea kufanywa katika msitu wa Chome Shengena.

Mh Lugola amesema kuwa msitu huo umekuwa ukiharibiwa na wananchi wanaofanya shughuli za kibinadamu ikiwemo kilimo pamoja na uchimbaji wa madini ambapo ili kuhakikisha mazingira ya msitu huo yanarudi katika hali yake ya kawaida serikali iliamua kupanda miti hiyo na kugawa miti mingine ya asili.

Ameongeza kuwa mbali na kupandwa kwa miti hiyo serikali pia imeweka ulinzi katika msitu huo ili kuzuia shughuli za kibinadamu ambapo ulinzi huo unafanywa na askari kutoka jeshi la kujenga taifa (JKT).

Hata hivyo naibu waziri huyo amewataka viongozi wote waliopewa mamlaka kote nchini kusimamia sheria na taratibu zilizowekwa za utunzaji wa mazingira hapa nchini.

MITI ELFU MBILI MIA TANO IMEPANDWA KATIKA MSITU WA CHOME SHENGENA MITI ELFU MBILI MIA TANO IMEPANDWA KATIKA MSITU WA CHOME SHENGENA Reviewed by safina radio on April 25, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.