VIJANA WATAKIWA KUFANYA KAZI BADALA YA KUKAA VIJIWENI


Vijana Mkoani Iringa wametakiwa kufanya kazi kwa bidii na kuondokana na tabia ya kukaa vijiweni ili kuunga mkono juhudi za Rais Dk. John Magufuli za kupambana kuhakikisha Tanzania inakuwa nchi ya viwanda kwa faida ya wananchi wote.

Image result for PICHA YA VIJANA WAKIFANYA KAZI


Hayo yamesemwa na Mkuu wa Mkoa wa Iringa Bi Amina Masenza wakati wa Tamasha lililoandaliwa na baadhi ya wasanii wa filamu ambao wako mkoani Iringa kwaajili ya kutoa  elimu kwa vijana kuachana na tabia ya kutumia muda mwingi vijiweni.

Aidha, Masenza amesema kuwa Mkoa wa Iringa utajengwa na wanairinga endapo watajituma na kufanyakazi ili kuufanya mkoa huo kuwa mkoa wa viwanda.

Kwa upande wake mkuu wa wilaya Iringa Bw Richard Kasesela amesema kuwa watapambana kuhakikisha kuwa wanazidi kuwapa elimu vijana ili wahamasike kufanya kazi.

Hata hivyo, zaidi ya wasanii sitini wako mkoani Iringa kutoa elimu kwa vijana mbali mbali kuachana na tabia ya kukaa vijiweni ambapo kaulimbiu yao ni amka kijana tujenge nchi yetu.




VIJANA WATAKIWA KUFANYA KAZI BADALA YA KUKAA VIJIWENI VIJANA WATAKIWA KUFANYA KAZI BADALA YA KUKAA VIJIWENI Reviewed by safina radio on April 16, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.