ZIMBABWE KUSHIRIKI MKUTANO WA JUMUIYA YA MADOLA.
Zimbabwe itashiriki katika Mkutano wa viongozi wa
nchi kutoka muungano wa Jumuiya ya Madola unaofanyika wiki hii jijini London
nchini Uingereza.
RAIS WA ZIMBZBWE EMMERSON MNANGAGWA |
Itakuwa mara ya kwanza kwa Zimbabwe kurejea katika
mkutano huo baada ya kufungiwa mwaka 2003 kwa sababu ya wizi wa kura na
ukiukwaji wa haki za binadamu chini ya uongozi wa aliyekuwa rais wa nchi hiyo Robert
Mugabe.
Zimbabwe haijaalikuwa kuhudhuria mkutano wa Jumuiya
ya Madola tangu nchi hiyo kuzuiliwa kwa vikao vyote vya jumuiya hiyo tangu
mwaka 2003 kufuatia matokeo ya uchaguzi wa rais, mnamo mwezi Machi mwaka 2002.
Kadhalika Muungano wa Ulaya ulitangaza vikwazo dhidi
ya nchi hiyo.
Kwa mujibu wa makisio ya wachunguzi wa kimataifa, wakati huo
Mugabe alishinda kwa matumizi ya mabavu, vitisho dhidi ya upinzani na ulaghai
katika uchaguzi.
ZIMBABWE KUSHIRIKI MKUTANO WA JUMUIYA YA MADOLA.
Reviewed by safina radio
on
April 17, 2018
Rating:
No comments