TAKUKURU MKOANI KILIMANJARO YAKAMILISHA UCHUNGUZI WA TUHUMA DHIDI YA KIWANDA CHA KUKOBOA KAHAWA.


Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa TAKUKURU mkoani Kilimanjaro imekamilisha uchunguzi wa tuhuma dhidi ya kiwanda cha kukoboa kahawa cha Tanganyika Coffee Cawe On TCCO.

Image result for PICHA YA NEMBO YA TAKUKURU



Akizungumza mkoani humo Kaimu Mkuu wa TAKUKURU wa mkoa huo Bw Mosess Obuda amesema kuwa tayari mafaili sita yamesha wasilishwa kwa mkurugenzi wa Mashtaka kwa ajili ya kuyaombea kibali cha kuwapeleka watuhumiwa mahakamani.

Aidha amesema kuwa muda sio mrefu taasisi hiyo itapata majibu ambayo taasisi na wananchi wanatarajia kuwa haki ya wananchi wa Moshi na wanachama wa vyama vya ushirika ambapo kitu kikubwa ni mali za wanachama wa ushirika huku akisema kuwa moja ya malalamiko yaliyofanyiwa uchunguzi ni ubadhirifu wa fedha za manunuzi ya mashine mpya.

Hata hivyo ameongeza kuwa TAKUKURU bado inaendelea kuwatafuta washtakiwa wawili wa Halmashauri ya Wilaya ya Hai ambao ni aliyekuwa Afisa Utumishi Faraja Ndatu na Afisa Uchumi Isaya Bayege kwa tuhuma za Kughushi vitambulisho na kujipatia mkopo wa fedha shilingi milioni thelathini na tano kutoka Benki ya CRDB.

Naye Afisa Mkuu wa TAKUKURU Mkoani humo Benedict Mongela amesema kuwa kwa kipindi cha miaka mitatu wameokoa fedha shilingi milioni tisa ambazo zilikuwa hazijatolewa risiti.

Hata hivyo, mwaka 2016 Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Mkoani Kilimanjaro ilipokea malalmiko ya uwepo wa ubadhirifu wa fedha katika kiwanda hicho.

TAKUKURU MKOANI KILIMANJARO YAKAMILISHA UCHUNGUZI WA TUHUMA DHIDI YA KIWANDA CHA KUKOBOA KAHAWA. TAKUKURU MKOANI KILIMANJARO YAKAMILISHA UCHUNGUZI WA TUHUMA DHIDI YA KIWANDA CHA  KUKOBOA KAHAWA. Reviewed by safina radio on April 13, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.