RAIS MAGUFULI ASEMA SERIKALI YAKE ITAILINDA MUUNGANO KWA NAMNA YOYOTE.9
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania Mh John
Joseph Magufuli amesema kuwa serikali ya
Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania itaulinda Muungano
kwa namna yeyote
pamoja na kuwadhibiti wale wote watakaojaribu kuvunja
Muungano wa Tanganyika
na Zanzibar.
Tamko hilo
amelitoa leo wakati akihutubia kwenye
sherehe ya maadhimisho ya miaka
54 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar
katika viwanja vya Jamhuri jijini Dodoma.
Mh Rais
amesema kuwa kamwe serikali haitamwonea aibu , huruma wala kumruhusu mtu yeyote kuvuruga amani na kuvunja
Muungano wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania.
Aidha Mh Rais
wakati akihutubia katika
sherehe hiyo ameeleza baadhi ya Manufaa ya Muungano wa Jamhuri ya
muungano wa Tanzaania
katika kipindi cha
miaka 54 tangu 1964 hadi 2018
ambapo amesema kuwa kama atatokea mtu yeyote au kundi au chama chochote kujaribu kuvunja Muungano hawataonewa huruma
iwe wa hapa nchini au nje kwani amani ni msingi wa maendeleo.
Hali kadhalika
Katika kipindi cha
miaka 54 baadhi ya
huduma za jamii zilizoimarishwa katika Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania katika Nyanja za
kiuchumi kisiasa na
kijamii ni pamoja na miundombinu ya umeme ,usafiri wa nchi kavu na majini,upatikanaji wa huduma za
jamii kama elimu, afya ,na baadhi ya huduma za elimu na afya kuongezeka mara
dufu.
Hata hivyo Kauli
mbiu ya sherehe
ya Muungano wa
Tanzania inasema “ Miaka
54 ya Muungano wetu ni
mfano wa kuigwa
duniani tuuenzi, tuulinde , tuuimarishe
na kuudumisha kwa maendeleo
ya taifa letu” .
RAIS MAGUFULI ASEMA SERIKALI YAKE ITAILINDA MUUNGANO KWA NAMNA YOYOTE.9
Reviewed by safina radio
on
April 26, 2018
Rating:
No comments