MADAKTARI NCHINI DRC WAENDELEA NA MGOMO


Madaktari nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo wanaendelea na mgomo wao walioanza siku ya jana kutokana na wito uliotolewa na  chama chao kikuu.
Image result for BENDERA YA DRC
Madaktari nchini DR Congo wanaomba serikali kuboresha mishahara yao, huku wakiishutumu kutoheshimu makubaliano walioafikiana mwaka jana kuhusu madai yao.
Aidha wanadai kupewa mshahara mzuri, malipo ya kazi zao za ziada, kutambuliwa kwa vyeo vyao na ufumbuzi kwa madaktari mia moja waliyofukuzwa kinyume cha sheria mwaka 2016  na ambao wamefanya kazi tangu wakati huo bila malipo.
Wagonjwa wameomba madaktari kusitisha mgomo huo wakisema kuwa unawaathiri pakubwa, huku wakiomba serikali kutafutia ufumbuzi madai ya madaktari.
Mwishoni mwa wiki iliyopita, serikali imetoa mapendekezo kwa madaktari wanaogoma na tayari imejibu madai ya madaktari hao, huku ikisema kazi kubwa kwa sasa iko upande wa chama kikuu cha madaktari, ambacho hakikuwasilisha mapendekzo hayo kwa wanachama wake.



MADAKTARI NCHINI DRC WAENDELEA NA MGOMO MADAKTARI NCHINI DRC WAENDELEA NA MGOMO Reviewed by safina radio on April 24, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.