SERIKALI IMESEMA KUWA BADO KUNA UWEPO WA VIASHIRIA VYA HATARI KATIKA MAZIMGIRA.


Serikali imesema kuwa licha ya juhudi mbali mbali zinazoendelea kukabiliana na uharibifu wa mazingira na tabia nchi bado hali inaonesha kuwepo kwa viashiria vya hatari hivyo jamii na taasisi hazina budi kushirikiana ili kuokoa hali ya mazingira.

Image result for Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira January Makamba
Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira January Makamba.
Taarifa hiyo imekuja kufuatia hotuba ya bajeti ya Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira January Makamba wakati akizungumzia hifadhi endelevu ya mazingira bungeni mjini Dodoma.

Mh Makamba amesema kuwa kutokana na Sekta zote za maendeleo ya mwanadamu kutegemea mazingira, hali ya mazingira imeendelea kuonesha taswira ya kuwa jangwa hivyo jitihada zinahitajika ili kukabiliana na hali hiyo.

Aidha, amesema kuwa zipo bidii mbali mbali zinazofanyika na serikali katika kuhakikisha kuwa mazingira yanakuwa katika hali nzuri ikiwemo sera na sheria za mazingira kuendelea kusimamiwa kikamilifu pamoja na miradi ya usimamizi wa mazingira kwa mujibu wa sheria na sera zilizopo.

Nayo kamati ya kudumu ya bunge ya viwanda biashara na mazingira imeishauri serikali kuendelea kusimamia sheria na sera ya mzingira kikamilifu katika maeneo mbalimbali nchini.

SERIKALI IMESEMA KUWA BADO KUNA UWEPO WA VIASHIRIA VYA HATARI KATIKA MAZIMGIRA. SERIKALI IMESEMA KUWA BADO KUNA UWEPO WA VIASHIRIA VYA HATARI KATIKA MAZIMGIRA. Reviewed by safina radio on April 18, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.