SERIKALI INAMPANGO MAHUSUSI KWA ZAO LA ALIETI.


Serikali imesema kuwa imeweka mkakati mkubwa wa kuhakikisha kuwa zao la alizeti linazalishwa kwa wingi ili mafuta ya kutosha yaweze kupatikana na kusaidia kukuza uchumi wa nchi pamoja na wakulima wa maeneo yanaozalisha zao hilo.

Image result for ZAO LA ALIZETI.
Zao la Alizeti.
Hayo yamebainishwa bungeni mjini Dodoma na waziri wa kilimo Dk. Charles Tizeba wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalumu Mh. Matha Mlata kwa niaba ya waziri wa Viwanda Biashara na Uwezeshaji aliyetaka kujua kwanini  ruzuku za mbegu ya zao la alizeti hazijatolewa kwa wakulima ili kukidhi haja ya viwanda vinavyojengwa mkoani Singida.

Image result for dk. charles tizeba
Dk. Charles Tizeba.
Aidha, amesema kuwa serikali ina mkakati mahususi kwa zao la alizeti ambapo mkakati huo mbali na mambo mengine unalenga kuongeza uzalishaji wa zao la alizeti hapa nchini pamoja na usindikaji wa mazao yanayotokana na zao hilo.
Image result for ZAO LA ALIZETI.
Usindikaji wa zao la Alizeti.
Dkt Tizeba amesema kuwa mkakati huo umeanza ili kuhakikisha kuwa upatikanaji wa mbegu bora za alizeti unakuwa na utoshelevu ambapo aina nne za alizeti tofauti mpya zimekwisha kupatikana ambazo ni bora kuliko mbegu zilizokuwa zikitumika nchini kwa muda mrefu.
Image result for ZAO LA ALIZETI.
Varayati za aina ya mbegu za alizeti.
Hata hivyo amesema kuwa, awali mbegu zenye kuzalisha mafuta mengi kwa sasa zimepatikana katika aina nne na hivyo zitaanza kusambazwa kwa wakulima hapa nchini huku lengo lake likiwa ni kuzalisha malighafi za kutosha kwa ajili ya viwanda vinavyojengwa nchini.

SERIKALI INAMPANGO MAHUSUSI KWA ZAO LA ALIETI. SERIKALI INAMPANGO MAHUSUSI KWA ZAO LA ALIETI. Reviewed by safina radio on April 18, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.