RAYMOND MUSHI AWATAKA WANANCHI KUACHA KUHUJUMU MIUNDOMBINU YA MAJI ILI KUIMARISHA MAENDELEO MBALI MBALI KIJAMII.


Wananchi wa kijiji cha Sangara katika kata ya Riroda wilayani Babati mkoani Manyara wametakiwa kuacha kuhujumu  miundo mbinu ya maji badala yake watumie fursa ya  kupatikana kwa maji kuvutia maendeleo ikiwemo kuimarisha makazi bora, usafi wa mazingira na matumizi ya vyoo bora.

Akitambulisha mradi  mpya wa majaribio wa maji na usafi wa mazingira katika kijiji cha Sangara Mkuu wa wilaya ya Babati Raymond Mushi amesema kuwa  ni muhimu wakatambua kuwa miradi inayojengwa na serikali kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo ni miradi yao na kwamba ni lazima kuilinda,kusimamia na kuiendeleza.

Image result for Mkuu wa wilaya ya Babati Raymond Mushi
Mkuu wa Wilaya ya Babati Raymond Mushi.
Amefafanua kuwa kuongezeka kwa idadi ya watu katika maeneo mengi duniani kunaongeza pia matumizi makubwa ya maji jamii inatakiwa iangalie ajenda ya maji kuwa ya kudumu ili kunusuru jamii husika na ukosefu wa maji.

Kwa mujibu wa Bw Mushi migogoro mingi ya wakulima na wafugaji mkoani Manyara inatokana na watu kupigania maji hivyo wananchi wa kijiji cha Sangara wanatakiwa kushirikiana na wataalamu katika ujenzi wa miundo mbinu hiyo nakuwa tayari kuchangia gharama za maji wakati ukifika.

Naye Mkurugenzi Mkaazi wa shirika la Water Aid Tanzania Dr. Ibrahim Kabole amesema kuwa mradi huo wa majaribio katika kijiji cha Sangara unatekelezwa kwa miezi 24 kuanzia tarehe 15 Novemba 2017 hadi 31 Oktoba 2019 kwa ushirikiano wa Halmashauri ya wilaya ya Babati, shirika la Habitat for Humanity (HFHT),UTT Micro Finance,na Water pay limited ambapo unatarajia kuwahudumia wananchi,2700.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa kijiji cha Sangara, Martin Masong’ ameishukuru serikali kupitia shirika la Water Aid Tanzania kuondoa kero ya maji kwa kijiji hicho na vijiji jirani kwani walikuwa wakitumia punda kwenda umbali wa kilomita 8 kutafuta maji.

RAYMOND MUSHI AWATAKA WANANCHI KUACHA KUHUJUMU MIUNDOMBINU YA MAJI ILI KUIMARISHA MAENDELEO MBALI MBALI KIJAMII. RAYMOND MUSHI AWATAKA WANANCHI KUACHA KUHUJUMU MIUNDOMBINU YA MAJI ILI KUIMARISHA MAENDELEO MBALI MBALI KIJAMII. Reviewed by safina radio on April 12, 2018 Rating: 5

No comments