VIONGOZI WA KOREA KUSINI NA KASKAZINI WAKUTANA


Kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong Un na Rais wa Korea Kusini Moon Jae-in wanafanya mkutano wa kilele wa kihistoria, baada ya kupeana mikono katika eneo la mstari wa kijeshi ambao unazitenganisha nchi zao, katika ishara yenye ujumbe mkubwa.
Rais w a Korea kaskazini Kim jong un na mwenzake wa Kusini Moon Jae-in
KIM KUSHOTO NA MOON KULIA
                 
 Kim alimwambia Moon kuwa ana furaha kukutana naye, kabla ya mgeni huyo kuvuka upande wa Korea Kusini, na hivyo kuwa kiongozi wa kwanza wa Korea Kaskazini kukanyaga Kusini tangu vita vya Korea vilipomalizika miaka 65 iliyopita.

 Kutokana na mwaliko wa Kim, viongozi hao wawili walivuka na kuingia upande wa Kaskazini huku wakiwa wameshikana mikono kabla ya kuingia katika Jumba la Amani upande wa Kusini wa kijiji cha Panmunjom kwa ajili ya mkutano wao wa kilele ambao ni wa tatu wa aina hiyo tangu uhasama ulipositishwa mwaka 1953.

Hata hivyo Kim amemwambia Moon kuwa mkutano huo ni mwanzo wa historia mpya ambapo Moon alimjibu akisema anatumaini kuwa watafikia makubaliano muhimu ili kuwapa zawadi watu wote wa Korea na watu wanaotaka amani.
                                





VIONGOZI WA KOREA KUSINI NA KASKAZINI WAKUTANA VIONGOZI WA KOREA KUSINI NA KASKAZINI WAKUTANA Reviewed by safina radio on April 27, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.