WALIOVAMIA ENEO LA RELI WAANZA KUPEWA ELIMU
Shirika la Reli Nchni TRL limeanza kutoa elimu kwa
watu waliovamia maeneo ya reli ndani ya mita thelathini kusogea mbali na maeneo
hayo ili kurahisishia serikali kutekeleza miradi miwili ya reli iliyokusudiwa
kwa manufaa ya taifa.
Mkuu wa Wilaya ya Kilosa Bw Adam Mgoyi amewataka
wafugaji wote waliovamia maeneo ya reli kuondoka haraka iwezekanavyo wakati
zoezi hilo la utoaji wa elimu kwa wananchi wa Kilosa linaendelea.
Kwa upande wa wafugaji waliovamia maeneo hayo
yanayomilikiwa na TRL wameomba serikali
iwatafutie maeneo mbadala ili wahamie na kupisha ujenzi wa reli hiyo.
Hata hivyo, Miradi ya reli ya kisasa katika kiwango
cha kimataifa na uboreshaji wa reli ya kati ambao unatarajiwa kuanza hivi karibuni
ukiwa katika awamu mbili yaani kuanzia Dar es salaam hadi Kilosa na Kilosa hadi
Isaka.
WALIOVAMIA ENEO LA RELI WAANZA KUPEWA ELIMU
Reviewed by safina radio
on
April 27, 2018
Rating:
No comments