UPO UMUHIMU WA KUFANYA MAOMBI YA KUHARIBU ROHO YA MAUTI NDANI YA NDOA.
Jamii imetakiwa kufahamu kuwa kuna umuhimu mkubwa wa
kufanya maombi ya kuharibu roho mauti kwenye ndoa kwani roho hiyo imekuwa
ikiwatesa wengi kiuchumi,kiafya na mara nyingine kusababisha ndoa kuvinjika.

Huduma ya redio safina kesho katika ukumbi wa maombi
uliopo mbauda jijini Arusha kuanzia saa mbili asubuhi hadi saa saba mchana
imeandaa maombi maalumu ya kushughulikia roho ya mauti kwenye ndoa pamoja na
uchumba ili kurejesha mahusiano mazuri.
Aidha kwa mujibu wa somo hilo adui anapopata mwanya
kwenye ndoa huachilia roho ya mauti kwenye maeneo mbalimbali kama vile afya,
biashara,kilimo,ufugaji,lengo likiwa ni kuharibu maendeleo pamoja na mahusiano
ya wanandoa.
Pia maombi hayo yatakwenda samabamba na maombi ya
kurejesha mahusiano ya uchumba uliovunjika kwa kuwaombea vijana wanaotarajia
kuingia kwenye ndoa ili wakaanze maisha bila kusumbuliwa na roho ya mauti inayovuruga
ndoa nyingi kwa sasa.
Hata hivyo wanandoa kesho watafundishwa namna ya
kuzijua dalili za roho ya mauti pamoja na kuzishughulikia ili kunusuru
mahusiano na uchumi wa familia na elimu ambayo imekuwa ikisuasua kwa watoto
baada ya ndoa kuvunjika.
UPO UMUHIMU WA KUFANYA MAOMBI YA KUHARIBU ROHO YA MAUTI NDANI YA NDOA.
Reviewed by safina radio
on
April 20, 2018
Rating:

No comments