RAIS MAGUFULI AAPISHA VIONGOZI ALIOWATEUA HIVI KARIBUNI.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani Mh. Dk. John Magufuli leo amewaapisha viongozi mbali mbali aliyowateua wiki iliyopita wakiwemo majaji 10 wa mahakama kuu ya Tanzania.

Image result for KUAPISHWA KWA MAJAJI 10 NA NAIBU MWANASERIA MKUU WA SERIKALI IKULU

Hafla ya  kuapishwa kwa viongozi hao imefanyika Ikulu jijini Dar es salaam ambapo viongozi walioapishwa ni pamoja na majaji 10 wa mahakama kuu, Naibu Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Naibu Wakili Mkuu wa Serikali na Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka.

Aidha Rais Magufuli amewaasa Majaji hao kumtanguliza Mungu mbele pamoja na Tanzania ili kuamua mashauri kwa uweledi huku akidokeza kuwa kwa sasa Tanzania ipo katika vita vya kiuchumi.

Akizungumza katika hafla hiyo Waziri wa Katiba na Sheria Prof. Palamagamba Kabudi amesema kuwa kazi ya kuhukumu si kazi ya  nyepesi bali kunahitaji uaminifu pamoja na kutenda haki katika kutoa maauzi bila upendeleo.

Naye Jaji Mkuu wa Tanzania Ibrahim Juma amesema kuwa mzigo wa kusikiliza mashauri umepungua kutoka mashauri 535 hadi 460 kwa mwaka,huku wastani wa kusikiliza mashauri kwa jaji mmoja kwa mwaka ikiwa ni mashauri 178 lakini ambapo wastani uliowekwa na mahakama kwa sasa ya kusikiliza mashauri kwa jaji mmoja kwa mwaka ni mashauri 220.

RAIS MAGUFULI AAPISHA VIONGOZI ALIOWATEUA HIVI KARIBUNI. RAIS MAGUFULI AAPISHA VIONGOZI ALIOWATEUA HIVI KARIBUNI. Reviewed by safina radio on April 20, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.