DKT. SIMON CHACHA AWATAKA VIONGOZI WA SIASA KUTOKA JUMUIYA YA WAZAZI KURUDISHA MAADILI KWA WATOTO.
Katika kuadhimisha siku ya watoto wanaoishi na
kufanya kazi mtaani Duniani,Mkoani Arusha maadhimisho hayo yameadhimishwa kwa
ushirikiano wa asasi mbalimbali pamoja na Halmashauri ya jiji la Arusha ambapo
Mganga Mkuu wa jiji Dkt.Simon Chacha amewataka viongozi wa vyama vya siasa
walioko katika jumuiya za wazazi kurudisha maadili kwa watoto.
Ameyasema hayo leo wakatika alipokuwa mgeni rasmi
katika maadhimisho hayo ambayo yameandaliwa na kituo cha Amani Children Home ambapo
amewataka viongozi wa dini mbalimbali kuhubiri malezi bora ya watoto kwa wazizi
na kuhakikisha maadili mazuri yanatekelezwa.
Aidha Dkt Chacha amesema kuwa serikali itahakikisha
inawajali watoto hao kwa kuwapatia malazi na tiba bora huku akiwaomba wadau wa
maendeleo ya watoto kujitoa kwa wingi katika kuwasaidia watoto ambao wanakubwa
na majanga mbalimbali yakiwemo ubakaji,ulawiti na unyanyasaji wa jinsia thidi
yao.
Naye Afisa Ustawi wa jamii jiji la Arusha Bi Martha
George amesema kuwa watoto wanaoishi na kufanya kazi mitaani ni kundi ambalo
linatambuliwa kwa mujibu wa sheria ya mtoto namba 21 ya mwaka 2009 kifungu cha
16 juu ya kupatiwa ulinzi na kupata matunzo na haki zao za msingi.
Awali akisoma risala mbele ya mgeni rasmi mtoto
Milton Aminiel amesema kuwa zipo sababu zinazomfanya mtoto kuingia mtaani moja
wapo ikiwa ni unyanyaswaji majumbani,ugomvi wa wazazi,kutelekezwa na wazazi au
walezi,umaskini,vifo vya wazazi,ushawishi wa makundi rika pamoja na sababu za dini
pamoja na kimila na desturi.
DKT. SIMON CHACHA AWATAKA VIONGOZI WA SIASA KUTOKA JUMUIYA YA WAZAZI KURUDISHA MAADILI KWA WATOTO.
Reviewed by safina radio
on
April 12, 2018
Rating:
No comments