BENDERA YA SYRIA YAPEPEA KATIKA MJI WA DOUMA.
Wizara ya ulinzi ya Urusi imesema bendera ya utawala wa Syria
inapeperuka katika mji wa Douma ulioko katika eneo la Ghouta Mashariki, hiyo
ikiashiria kuwa majeshi ya utawala wa Syria yana udhibiti kamili wa Ghouta
Mashariki.
Mkuu wa kituo cha
maridhiano cha jeshi la Urusi nchini Syria, Meja Jenerali Yury Yevtushenko
amesema leo ni siku ya kihistoria nchini Syria kwani kupeperushwa kwa bendera
ya utawala wa Syria ni ishara tosha ya udhibiti kamili wa mji wa Douma na
Ghouta Mashariki nzima.
Serikali ya Syria yenyewe bado haijatangaza rasmi kuwa
inaidhibiti Douma ambao ulikuwa ngome ya mwisho ya waasi katika eneo la Gouta
Mashariki, huku Wizara ya ulinzi ya ikimesema wanajeshi wake wameanza kushika
doria katika mji huo.
Hata hivyo Shirika la kutetea haki za binadamu Syria limesema
waasi wa kundi la Jaish al Islam wamesalimisha silaha zao nzito na kiongozi wao
Issam Buwaydani ameondoka Douma.
BENDERA YA SYRIA YAPEPEA KATIKA MJI WA DOUMA.
Reviewed by safina radio
on
April 12, 2018
Rating:
No comments