wananchi wanaosumbuliwa na changamoto mbalimbali za kimaisha watakiwa katika ofisi za ustawi wa jamii kupatiwa ushauri.


Naibu waziri wa afya maendeleo ya jamii jinsia wazee na watoto Mh Faustine Ndugulile amewataka wananchi wanaosumbuliwa na changamoto mbalimbali za kimaisha ikiwemo msongo wa mawazo kufika katika ofisi za maafisa ustawi wa jamii walioko katika kila wilaya ili kupata ushauri wa kisaikolojia ili waondokane na matatizo hayo.

Image result for picha ya naibu waziri wa afya faustine ndugulile
MH. NDUGULILE
Mh Ndugulile ameyasema hayo leo bungeni mjini Dodoma wakati akijibu swali la mbunge wa viti maalumu Mh Fatma Hassan Towfik aliyetaka kujua serikali inawasaidiaje wananchi ambao wanakabiliwa na matatizo mbalimbali ya kimaisha na kuwafanya kukata tamaa ya kuishi.

Amesema kuwa wananchi wengi hapa nchini wanakabiliwa na msongo wa mawazo unaosababishwa na sababu za kimaisha ikiwemo umaskini,kutengwa,kunyanyapaliwa,magonjwa na upweke na kuwafanya kukata tamaa ya kuishi,hivyo ni bora wananchi wanapoona hali kama hiyo wakafika katika ofisi hizo ili kupata ushauri.

Aidha katika hatua nyingine naibu waziri huyo ameitaka jamii inayokumbw a na migogoro ya kifamilia kufika katika ofisi za ustawi wa jamii zilizopo katika kila halmashauri ili kupata ushauri wa kusuluhisha migogoro hiyo,ambapo huduma zinapatika siku zote za kazi.

wananchi wanaosumbuliwa na changamoto mbalimbali za kimaisha watakiwa katika ofisi za ustawi wa jamii kupatiwa ushauri. wananchi wanaosumbuliwa na changamoto mbalimbali za kimaisha watakiwa katika ofisi za ustawi wa jamii kupatiwa ushauri. Reviewed by safina radio on April 13, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.