SERIKALI INAENDELEA KUBORESHA VITUO VYA AFYA KWA KUWEKA HUDUMA ZA DHARURA.


Naibu waziri wa afya maendeleo ya jamii jinsia wazee na watoto Mh Faustine Ndugulile amesema kuwa serikali inaendelea kuboresha vituo vya afya kwa kuweka huduma za dharura ili kupunguza vifo vya akina mama na watoto njiti.

Image result for Mh Faustine Ndugulile

Mh Ndugulile ameyasema hayo leo bungeni jijini Dodoma wakati akijibu swali la nyongeza la mbunge wa viti maalumu Mh Halima Bulembo aliyetaka kujua kuwa serikali ina mpango gani wa kuboresha huduma za watoto njiti katika hospitali na vituo mbalimbali Vya afya.

Amesema kuwa vifo vya akina mama na watoto vimekuwa vingi hapa nchini na serikali kwa kulitambua hilo imejiwekea mkakati wa kuhakikisha kuwa huduma za watoto njiti na watoto wote zinapatikana katika hospitali zote,vituo vya afya na katika hospitali za wilaya.

Aidha katika hatua nyingine naibu waziri wa nchi ofisi ya rais TAMISEMI Mh Josephat Kandege amesema kuwa serikali inaendelea kushughulikia ombi la kuongeza muda likizo ya uzazi kwa wanawake wanaojifungua watoto njiti kutoka muda wa miezi mitatu hadi miezi sita.

Hata hivyo bunge la bajeti linaendelea jijini Dodoma ambapo leo waziri wa elimu sayansi tekinolojia na mafunzo ya ufundi Mh Joyce Ndalichako amewasilisha bajeti ya wizara yake kwa mwaka  wa fedha wa 2018/2019.

SERIKALI INAENDELEA KUBORESHA VITUO VYA AFYA KWA KUWEKA HUDUMA ZA DHARURA. SERIKALI INAENDELEA KUBORESHA VITUO VYA AFYA KWA KUWEKA HUDUMA ZA DHARURA. Reviewed by safina radio on April 30, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.