imebainika kuwa ili mtu afanikiwe ni lazima kujenga madhabahu kwa unachofanya.


Imebeinika kuwa kanuni moja wapo ya mtu kufanikiwa kiroho na kimwili ni pamoja na kuijengea madhabahu kila kitu anachokifanya kwa kumuweka Yesu Kristo moyoni mwake,kulisoma neno na kuomba, pamoja na kufanya kazi kwa bidii.

Image result for picha ya madhabahu

Redio safina kesho katika ukumbi wa maombi uliopo mbauda jijini Arusha kuanzia saa mbili asubuhi hadi saa sita mchana imeandaa mafundisho pamoja na maombi kuhusu madhabahu inavyoweza kuamua mafanikio ya mtu yawe mazuri au mabaya.

Kwa mujibu wa somo hilo baadhi ya watu katika jamii wamekuwa wakipitia kwenye changamoto nyingi kutokana na maisha yao kushikiliwa kwenye madhabahu ya miungu na kuwafanya kutumikia adhabu ya magonjwa,laana,madeni,umaskini huku wengine wakidhibitiwa wasimwabudu Mungu kwa viwango vya juu.

Aidha njia pekee ya kuweza kuondokana na nguvu ya madhabahu ya miungu na kumtumikia Mungu kwa viwango vya juu ni wajibu wa kila mtu kukaa mbele za Mungu kwa muda mrefu na kumshirikisha kile anachokifanya kama vile biashara,kilimo,ufugaji,masomo,pamoja na huduma kwa ujumla.

Hata hivyo kesho katika ukumbi wa safina redio kutafanyika maombi maalum ya kuwafungua watu dhidi ya magonjwa sugu,migogoro ya ndoa,madeni,laana,matatizo ya ajira,pamoja na ndoto mbaya zinazowasumbua watu kutokana na vifungo vya nguvu za kimadhabahu.

imebainika kuwa ili mtu afanikiwe ni lazima kujenga madhabahu kwa unachofanya. imebainika kuwa ili mtu afanikiwe ni lazima kujenga madhabahu kwa unachofanya. Reviewed by safina radio on April 13, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.