RAIS MAGUFULI LEO AMEZINDUA BARABARA YA KONDOA


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Dk. John Magufuli leo amezindua barabara ya Kondoa Mkoani Dodoma hadi Babati Mkoani Manyara yenye urefu wa kilomita 251 huku akiwataka wakuu wa vitengo vya ulinzi na usalama barabarani kusimamia sheria za barabarani ili kupunguza ajali za mara kwa mara.

Image result for picha ya rais magufuli
RAIS WA TANZANIA JOHN MAGUFULI.
Akizungumza wakati wa uzinduzi huo Rais Magufuli ameonya tabia ya madereva kuendesha magari wakiwa wamelewa na kutokuzingatia sheria za usalama barabarani huku akiwataka wananchi kutokuondoa alama za barabarani ili kuepusha kutokea kwa ajili zisizo za lazima.

Aidha amesema kuwa barabara hiyo ya Kondoa-Babati ni sehemu ya barabara ya kaskazini inayounganisha ukanada wa kusini na kaskazini mwa bara la Afrika amabapo nchi nane zimeunganishwa na barabara hiyo ikiwemo, Afrika Kusini, Kenya, Ethiopia, na Misri.

Kwa upande mwingine Dk. Magufuli amesema kuwa Benki ya Maendeleo ya Afrika imeahidi zaidi ya Dola Milioni 200 kwa ajili ujenzi wa uwanja wa ndege wa kisasa jijini Dodoma huku akiwataka waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Prf. Makame Mbarawa na Waziri wa Fedha Philip Mpango kufuatilia suala hilo.

Hata hivyo, ujenzi wa barabara hiyo umefadhiliwa na Shirika la Maendeleo ya Watu wa Japani JEIKA na Benki ya Maendeleo ya Afrika ambapo rais wa benki ya maendeleo ya Afrika Bw Akinumwi Adesina amesema kuwa barabara hiyo itakuza uchumi wa Tanzania kutokana na kurahisisha shughuliza za kibiashara katika ukanda wa maziwa makuu.



RAIS MAGUFULI LEO AMEZINDUA BARABARA YA KONDOA RAIS MAGUFULI LEO AMEZINDUA BARABARA YA KONDOA Reviewed by safina radio on April 27, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.