TFDA YAGUNDUA KUWEPO NA MBINU YA WAFANYABIASHARA KUWEKA VIPODOZI MADUKA YA KUUZIA VIFAA VYA UJENZI.


Vipodozi vilivyopigwa marufuku vyenye kugharimu fedha zaidi ya shilingi milioni tano vimekamatwa katika baadhi ya maduka katika Manispaa ya Tabora baada ya mamlaka husika kufanya operesheni maalumu ya kutafuta vipodozi vilivyopigwa marufuku.

Image result for tfda

Meneja wa Mamlaka ya Chakula na Dawa TFDA Kanda ya Magharibi Dk. Edga Mahundi amesema kuwa wamegundua kuwepo na mbinu ya wafanya biashara kuweka vipodozi vilivyopigwa marufuku kwenye maduka ya kuuzia vifaa vya ujenzi jambo ambalo ni kosa kisheria.

Miongoni wa wauzaji waliokamatwa wakiuza vipodozi vilivyopigwa marufuku ni pamoja na Babuu Mwacha na Jesca Baraka waliokiri kufanya makosa na kuahidi kutokurudia tena kosa hilo.

Naye Dk. Mahundi amesema kuwa wametoa elimu na mafunzo mbali mbali kwa wauzaji wa vipodozi ,chakula na dawa kwa lengo la kuwafanya watambue madhara ya kuuza vipodozi vilivyopigwa marufuku huku mamlaka ikiwataka wauzaji kufuata sheria kanuni na taratibu za uuzaji wa bidhaa zao .

Hata hivyo ametoa wito kwa wananchi kuwafichua wauzaji wanaokiuka sheria zilizowekwa katika biashara zao ili kupatikana kwa bidhaa na huduma zinazokidhi viwango na vigezo kwa afya za walaji.

TFDA YAGUNDUA KUWEPO NA MBINU YA WAFANYABIASHARA KUWEKA VIPODOZI MADUKA YA KUUZIA VIFAA VYA UJENZI. TFDA YAGUNDUA KUWEPO NA MBINU YA WAFANYABIASHARA KUWEKA VIPODOZI MADUKA YA KUUZIA VIFAA VYA UJENZI. Reviewed by safina radio on April 18, 2018 Rating: 5

No comments

Support

Need our help to upload or customize this blogger template? Contact me with details about the theme customization you need.