MAHAMMADU BUHARI ATAKUWA RAIS WA KWANZA KUZURU MAREKANI TANGU DONALD TRUMP KUSHIKA HATAMU ZA MADARAKA.
Rais wa Nigeria Muhammadu Buhari anatarajia kuzuru Marekani
Jumatatu hii ikiwa ni ziara rasmi ya
kwanza kwa rais wa nchi ya Afrika tangu Rais wa Marekani Donald Trump kuchukua
madaraka nchini Marekani.
![]() |
Rais wa Nigeria Muhammadu Buhari kushoto na Rais wa Marekani Donald Trump kulia. |
Ziara ya Muhammadu Buhari inakuja baada ya ile ya rais wa
Ufaransa, Emmanuel Macron na Kansela wa Ujerumani Angela Merkel nchini
Marekani.
Mkutano kati ya Rais Buhari na mwenyeji wake Donald Trump
utazingatia masuala ya usalama na uchumi.
Mwaliko huo ulitolewa mnamo mwezi Januari 2017, Baada ya Donald
Trump kukabidhiwa madaraka ya uongozi wa nchi alimpigia simu mwenzake wa
Nigeria, Muhammadu Buhari, na kumuomba azuru Marekani.
Muhammadu Buhari atakuwa kiongozi wa kwanza wa taifa kutoka bara
la Afrika kulakiwa na Rais wa Marekani Donald Trump katika ikulu ya White House,ambapo
atakapokutana na kiongozi huyo kwa mashauriano rasmi mjini Washington.
Hata hivyo Kwa mujibu wa ikulu ya White House, mazungumzo kati
ya wawili hao yatajikita kuhusu vita dhidi ya ugaidi, usalama na uchumi,ambapo Ziara ya Rais Muhammadu Buhari inakuja ikiwa
zimesalia siku chache kabla ya uchaguzi wa urais nchini Nigeria.
MAHAMMADU BUHARI ATAKUWA RAIS WA KWANZA KUZURU MAREKANI TANGU DONALD TRUMP KUSHIKA HATAMU ZA MADARAKA.
Reviewed by safina radio
on
April 30, 2018
Rating:
No comments