IMEELEZWA KUWA MATUMIZI SAHIHI YA TEHAMA YATASAIDIA UKUAJI WA UCHUMI.
Waziri wa ujenzi uchukuzi na mawasiliano Prf. Makame
Mbarawa Mnyaa amesema kuwa matumizi sahihi ya vifaa vya kiteknolojia ya TEHAMA ikiwemo
simu za mkononi yatachangia ukuaji wa uchumi usioharibu mazingira.
MH.MBARAWA |
Waziri Mbarawa ameyasema hayo mjini Unguja kwenye
mkutano wa nane wa wiki ya kijani ambapo amesema kuwa lengo la mkutano huo nikujadiliana
namna ya kutumia TEHAMA ili kuendana na mabadiliko ya tabia nchi.
Aidha, amesema kuwa Tanzania inawatumiaji wa simu za
mkononi takribani milioni 42 na wanatumia vifaa mbali mbali vya kielektroniki
ambapo baada ya muda fulani vifaa hivyo huisha matumizi hivyo vinatakiwa
kutolewa kwenye soko kwa uangalifu mkubwa bila kuharibu mazingira kwa wanaotumia.
Amesema kuwa kutokana na wataalamu wa vifaa vya
kielektroniki kutoka Shirika la Mawasiliano Duniani ITU, Tanzania itajifunza utaalamu
huo unaotumika Duniani kuharibu vifaa hivyo vya kielektroniki vilivyopitwa na
muda wa matumizi yake.
Kwa upande wake Mkurugenzi wa Idara ya Mawasiliano na
Viwango vya Shirika hilo la Mawasiliano Duniani-ITU Dk. Chaesa Li amewataka wataalamu
wa TEHAMA kujadili namna bora ya kuchakata bidhaa na huduma za mawasiliano zilizopitwa
na wakati.
IMEELEZWA KUWA MATUMIZI SAHIHI YA TEHAMA YATASAIDIA UKUAJI WA UCHUMI.
Reviewed by safina radio
on
April 11, 2018
Rating:
No comments